Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP, DCI ‘wamkimbia’ Nondo mahakamani Dar
Habari za SiasaTangulizi

IGP, DCI ‘wamkimbia’ Nondo mahakamani Dar

Mawakili wa Abdul Nondo wakiwa Mahakama Kuu muda mchache baada ya kesi yao
Spread the love

WAKATI Mwenyekiti wa Mtandao wa Wananfunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo akipandishwa kizimbani leo asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam nayo imeanza kusikiliza kesi ya Nondo dhidi ya Serikali, akidai haki ya uwakilishi pamoja na dhamana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mawakili wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), na wale wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wakiongozwa na Mpoki Mpare na Jebra Kambole wamefika mbele ya Jaji Rehema Semeji na kuwasilisha mashtaka dhidi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mwanasheria Mkuu (AG) na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP).

Katika kesi hiyo namba 49 ya mwaka 2018, mawakili hao wameiomba mahakama kuiamuru serikali kutoa dhamana na kuruhusu haki ya uwakilishi kwa mteja wao Nondo.

Amesema, “Maombi haya yalifunguliwa dhidi ya DCI, IGP, AG tukiomba mahakama kutoa amri ya kuletwa mahakamani kwa mwanafunzi Nondo au kumuachia kwa dhamana kwani ameshikiliwa na polisi kwa muda mrefu bila sababu za msingi kutolewa”

Jaji Sameja ameutaka upande wa Jamhuri kujibu hoja za utetezi Machi 26, 2018.

Jaji Semeji amesikilia maombi hayo na kueleza kuwa shauri hilo litaendelea kusikilizwa Aprili 4 Mwaka huu.

Nondo ambaye ni Mwanafunzi wa Mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo Sayansi ya Siasa na Utawala amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa.

Na kusomewa mashtaka mawili na wakili wa serikali Abeid Mwandalamo mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, John Mpitanjia.

Mwandalamo Amedai kuwa kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa eneo la Ubungo Dar es Salaam na kuzisambaza kupitia mtandao wa kijamii wa Whatsapp kwamba yupo hatarini.

Katika shtaka la pili, ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma Mafinga alipokuwa anatoa taarifa kwa askari kwenye Kituo cha Polisi Mafinga kwa kusema kuwa alitekwa na watu wasiojulikana Dar es Salaam na kupelekwa kiwanda cha Pareto Mafinga. Hata hivyo, Nondo alikana mashtaka hayo.

Mwanadalamo amedai ushahidi bado haujakamilika hivyo wanaomba siku chache, kwa kipindi watakachokuwa wanafanya upelelezi mtuhumiwa asipewe dhamana.

Amedai kuwa kwa sababu bado wanafanya upelelezi kwa rafiki wake wa karibu, kama atapewa dhamana anaweza kuingilia na kuharibu upelelezi huo.

Hata hivyo Wakili wa utetezi, Chance Luwoga amesema mashtaka aliyosomewa Nondo yanaruhusu kupewa dhamana hivyo hakuna sababu za msingi za kuzuiliwa kwa dhamana ya mteja wake.

Hakimu Mpitanjia amesema kuwa Mahakama hiyo itatoa uamuzi juu ya dhamanda ya mshukiwa huyo tarehe 26 Machi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!