Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafuasi wa Mange Kimambi waanza kuwekwa mbaroni
Habari Mchanganyiko

Wafuasi wa Mange Kimambi waanza kuwekwa mbaroni

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

JESHI la polisi mkoa wa Dodoma linawashikilia watu wawili kwa makosa ya kutumia vibaya mitandao ya kijamii kwa madai ya kuchochea maandamano ya nchi nzima ambayo yanakusudiwa kufanyika Aprili 26 mwaka huu. Anaripoti Dany Tibason … (endelea). 

Maandamano hayo yaliyopangwa kufanyika Aprili 26 mwaka huu, yanayohamasishwa na Mange Kimambi anayeishi nchini Marekani kwa lengo la kupinga mwenendo wa nchi kwa sasa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema jeshi hilo limewakamata watu wawili ambao wanatumia vibaya mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuchochea maandamano nchi nzima kinyume na taratibu za nchi.

“Kwa muda mrefu sasa kwa makusudi na wakitambua kuwa ni kosa kisheria, baadhi ya watu wasiopenda amani na utulivu wa nchi wanatumia vibaya mitandao ya mawasiliano kuvunja sheria na kuhamasisha chuki dhidi ya serikali kuhamasisha maandamano yasiyo halali yenye viashiria vya kuvuruga amani ya nchi waliyopanga kuyafanya nchi nzima siku ya tarehe 26/4/2018.

“Hapa Dodoma tumekamatwa watu wawili ambao kwa makusudi kwa kutumia mitandao ya simu wanasambaza maneno yenye uchochezi dhidi ya serikali, wanatishia usalama wa nchi wanahamasisha maandamano ya nchi nzima yenye viashiria vya uvunjifu wa amani,” amesema Muroto.

Kamanda Muroto amewataja waliokamatwa kuwa ni Amandus Machali (31) dereva wa NHIF na mkazi wa Kigamboni geti jeusi jijini Dar es Salaam na Yuda Mbata (29), mkulima na mkazi wa kijiji cha Mpanatwa wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.

Katika tukio lingine Kamanda Muroto amesema kumetokea vifo vya watu watatu wa familia moja katika kijiji cha Gwandi katika wilaya ya Chemba mkoani Dodoma kutokana na watu hao kuangukiwa na ukuta wa nyumba wakiwa wamelala.

Amesema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 18, mwaka huu usiku katika kijiji hicho na kusema chanzo cha vifo hivyo ni kutokana na kuta za nyumba kulowana na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali mkoa wa Dodoma.

Aliwataja waliokufa kuwa ni Misa James (25) Happy James (2) na Mbalu James ambaye hakumtaja umri wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!