Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DPP amwachia huru Sadifa
Habari za SiasaTangulizi

DPP amwachia huru Sadifa

Aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dodoma imemwachia huru aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis baada ya Jamhuri kuwasilisha ombi la kuifuta kesi ya rushwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Sadifa ambaye ni mbunge wa Donge Zanzibar ameachiwa huru baada ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) kuamua kutoendelea na kesi hiyo.

Kifungu kinachompa mamlaka DPP kuamua kutoendelea na kesi yoyote ni 91(1) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai bila kuhojiwa na mamlaka yoyote.

Sadifa alituhumiwa kwa tuhuma za rushwa ya kuwataka wanachama wa CCM kumchagua Rashid Mohamed kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM katika uchaguzi wa uliofanyika mwezi Desemba mwaka jana.

Awali wa Sadifa alitiwa mbaroni Desemba 10 mwaka 2017  kwa tuhuma hizo na kupandishwa kizimbani Desemba 11, mwaka jana.

Shitaka la kwanza alidaiwa Desemba 9, 2017 katika makazi yake kwenye Kata ya Mnada mjini Dodoma akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM aliwahonga wanachama ili wamchague Rashid Mohamed aliyekuwa akiwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti katika uchaguzi mkuu wa umoja huo.

Sadifa katika shtaka la pili alidaiwa katika eneo hilo na siku hiyo hiyo, aliwaahidi kuwalipia usafiri wanachama wa umoja huo kuwasafirisha kutoka Dodoma hadi Kagera kama zawadi ili wamchague Rashid Mohamed aliyekuwa akiwania nafasi ya makamu mwenyekiti katika uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!