Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa DPP amwachia huru Sadifa
Habari za SiasaTangulizi

DPP amwachia huru Sadifa

Aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dodoma imemwachia huru aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis baada ya Jamhuri kuwasilisha ombi la kuifuta kesi ya rushwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Sadifa ambaye ni mbunge wa Donge Zanzibar ameachiwa huru baada ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) kuamua kutoendelea na kesi hiyo.

Kifungu kinachompa mamlaka DPP kuamua kutoendelea na kesi yoyote ni 91(1) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai bila kuhojiwa na mamlaka yoyote.

Sadifa alituhumiwa kwa tuhuma za rushwa ya kuwataka wanachama wa CCM kumchagua Rashid Mohamed kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM katika uchaguzi wa uliofanyika mwezi Desemba mwaka jana.

Awali wa Sadifa alitiwa mbaroni Desemba 10 mwaka 2017  kwa tuhuma hizo na kupandishwa kizimbani Desemba 11, mwaka jana.

Shitaka la kwanza alidaiwa Desemba 9, 2017 katika makazi yake kwenye Kata ya Mnada mjini Dodoma akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM aliwahonga wanachama ili wamchague Rashid Mohamed aliyekuwa akiwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti katika uchaguzi mkuu wa umoja huo.

Sadifa katika shtaka la pili alidaiwa katika eneo hilo na siku hiyo hiyo, aliwaahidi kuwalipia usafiri wanachama wa umoja huo kuwasafirisha kutoka Dodoma hadi Kagera kama zawadi ili wamchague Rashid Mohamed aliyekuwa akiwania nafasi ya makamu mwenyekiti katika uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!