Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko DC  atangaza vita na askari waliopiga raia
Habari Mchanganyiko

DC  atangaza vita na askari waliopiga raia

Askari Polisi wakiwa mtaani kukabiliana na wananchi. Picha ndogo Mkuu wa wilaya ya Ilala, Sophia Mjema
Spread the love

MKUU wa wilaya ya Ilala,  Sophia Mjema ameagiza kuchukuliwa hatua askari wanaodaiwa kuwapiga wananchi katika eneo la Gongo la mboto Jijini Dar es Salaam kwa madai ya kulipiza kisasi, anaandika Hamis Mguta.

Mjema amesema hayo leo alipokuwa akizungumza na wananchi hao wa Gongo la mboto ambao kwa siku tatu mfululizo wamekuwa wakishambuliwa na askari kwa kile kinachoelezwa kuwa walikuwa wanalipiza kisasi baada ya askari mwenzao kukutwa ameuawa.

“Kama Mkuu wa wilaya na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama jambo ambalo limefanyika kwa siku tatu hizo halikubaliki na kama kuna matatizo kati ya askari na raia kulikuwa kuna eneo la kupeleka matatizo hayo”

“Kama askari aliyekuwa amepatikana amefariki, utaratibu ilikuwa uchunguzi ufanyike ili kujiridhisha,” amesema Mjema.
Aidha, Mjema amesema wahusika wanatakiwa kuwachukulia hatua za kinidhamu askari waliofanya kitendo hicho.

“Askari walioshiriki kufanya jambo hili wachukuliwe hatua za kinidhamu na huko barabarani sitaki kumuona FFU yoyote anasumbua wananchi,” amesema.

Mmoja wa wananchi waliopigwa amesema tukio hilo lilitokea juzi saa mbili usiku ambapo askari hao walivamia maeneo mbalimbali, majumbani pamoja na maeneo ya biashara kisha kuanza kupiga watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!