Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Uchaguzi Mkuu Kenya washikiliwa na Mahakama
Kimataifa

Uchaguzi Mkuu Kenya washikiliwa na Mahakama

Spread the love

UCHAGUZI  Mkuu Nchini Kenya upo mashakani kufanyika Oktoba 26 kama ilivyotangazwa na Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo, (IEBC),  baada ya wapigakura kufungua kesi katika mahakama ya juu wakitaka uchaguzi usifanyike, anaandika Mwandishi wetu.

Leo kesi hiyo imeunguruma katika mahakama hiyo na kuahirishwa mpaka kesho asubuhi yatakapotolewa maamuzi kama uchaguzi huo utafanyika kama ulivyopangwa au la.

Mahakama ya juu nchini humo ilifuta uchaguzi mkuu na hivyo IEBC kutangaza Oktoba 26 kuwa siku ya Wakenya kushiriki katika uchaguzi wa marudio.

Wakati hayo yakiendelea nchini humo, mpinzani mkuu nchini humo, Raila Odinga ametangaza kujitoa katika uchaguzi huo kwa madai kuwa IEBC imeshindwa kutekeleza maagizo ya mahakama ya juu.

Hata hivyo, Rais Uhuru Kenyatta yeye amesisitiza kwamba lazima uchaguzi huo wa marudio ufanyike kama ulivyopangwa nchini humo na kwamba kila kitu kinaenda vizuri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!