Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uchaguzi Mkuu Kenya washikiliwa na Mahakama
Kimataifa

Uchaguzi Mkuu Kenya washikiliwa na Mahakama

Spread the love

UCHAGUZI  Mkuu Nchini Kenya upo mashakani kufanyika Oktoba 26 kama ilivyotangazwa na Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo, (IEBC),  baada ya wapigakura kufungua kesi katika mahakama ya juu wakitaka uchaguzi usifanyike, anaandika Mwandishi wetu.

Leo kesi hiyo imeunguruma katika mahakama hiyo na kuahirishwa mpaka kesho asubuhi yatakapotolewa maamuzi kama uchaguzi huo utafanyika kama ulivyopangwa au la.

Mahakama ya juu nchini humo ilifuta uchaguzi mkuu na hivyo IEBC kutangaza Oktoba 26 kuwa siku ya Wakenya kushiriki katika uchaguzi wa marudio.

Wakati hayo yakiendelea nchini humo, mpinzani mkuu nchini humo, Raila Odinga ametangaza kujitoa katika uchaguzi huo kwa madai kuwa IEBC imeshindwa kutekeleza maagizo ya mahakama ya juu.

Hata hivyo, Rais Uhuru Kenyatta yeye amesisitiza kwamba lazima uchaguzi huo wa marudio ufanyike kama ulivyopangwa nchini humo na kwamba kila kitu kinaenda vizuri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!