Wednesday , 17 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Josephine Mushumbusi atajwa kesi ya Lulu
Habari MchanganyikoMichezo

Josephine Mushumbusi atajwa kesi ya Lulu

Elizabeth Michael 'Lulu' (mwenye hauni jekundu) akiwa mahakamani. Picha ndogo Josephine Mushumbusi mmoja wa mashahidi wake
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemtaka askari aliyerekodi ushahidi wa Josephine Mushumbusi kufika mahakamani kutoa ushahidi kwenye kesi inayomkabili Elizabeth Michael (Lulu), anaandika Faki Sosi.

Mushumbusi ni mmoja wa mashahidi muhimu katika kesi ya msanii huyo ambaye alichukuliwa maelezo yake.

Lulu anatuhumiwa kumuua bila kukusudia msanii mwenzake aliyekuwa ana mahusiano naye kimapenzi, Steven Kanumba.

Leo katika mahakamani hiyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala aliwasilisha ombi la kusoma maelezo ya shahidi ambaye hayupo nchini na kwamba hataweza kupatikana.

Wakili wa serikali, Faraja George amepinga ushahidi huo kwa madi kwamba wakili wa utetezi hana mamlaka wala hawezi kufanya kazi ya ushahidi.

Baada ya mabishano hayo, Jaji Sam Rumanyika amesema kuwa ushahidi huo utatolewa na askari aliyerekodi maelezo ya shahidi ambaye ni sajent Nyange mwenye namba E103.

Katika hali isiyo ya kawaida Lulu alitimua mbio mara baada ya kutoka mahakamani huku sauti za ndugu zake zikisikia zikisema ‘Lulu kimbia’. Mshtakiwa huyo alikimbia kuzikwepa kamera za wanahabari waliokuwepo mahakamani hapo.

Kesi hiyo ambayo imesikilizwa mfululizo kuanzia wiki iliyopita itaendelea kesho Octoba 25.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Habari Mchanganyiko

Sekta binafsi yasifu utekelezaji wa Mkumbi

Spread the loveSERIKAL imepongezwa kwa utekelezaji wa mapendekezo ya sekta binafsi kupitia...

Habari Mchanganyiko

Kamati ya bunge yapigia chapuo kilimo ikolojia

Spread the loveSERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo imeshauriwa kushirikiana na wadau wa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili

Spread the loveSERIKALI imepata hasara ya kiasi cha Sh. 111.76 milioni, baada...

error: Content is protected !!