Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanaharakati wainuka na kupaza sauti
Habari Mchanganyiko

Wanaharakati wainuka na kupaza sauti

Mkuregenzi Mtendaji wa LHRC, Dk Hellen Kijo -Bisimba
Spread the love

KITUO cha  Sheria Haki za Binaadamu Nchini (LHRC), kimesema kwa sasa hali ya usalama hapa nchini ni siyo nzuri baada ya kuwapo matukio ya mashambulizi a silaha za moto, anaandika Faki Sosi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkuregenzi Mtendaji wa LHRC, Dk Hellen Kijo -Bisimba amesema tukio la hivi karibuni la kupigwa risasi  Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Tundu Lissu ni ishara mbaya katika masuala ya usalama.

Aidha, amesema kuwa mashambulizi mengine ni yake yaliyofanywa kwa kampuni ya mawakili ya  IMMMA ya jijini Dar es Salaam na kuharibu mali mbalimbali.

Mwanaharakati huyo amesema shambulio la kupigwa Lissu kwa Risasi limewastua na na kulilaani tukio hilo kwenye nchi.
Amesema kuwa shambulio la Lissu limetishia sana watetezi wa haki za binaadamu kutokana na Lissu kuwa mtetezi wa masuala mbalimbali hapa nchini.

Dk.Bisimba amesema  kuwa hivi Karibu kumetokea vitendo vya kutekwa kwa wananchi ndani ya nchi yao kufariki kwa Raia na Askari Kibiti Pwani .

Tukio lingine alilotaja la kuashiria uvunjifu wa amani ni tukio la hivi karibuni la kumtishia bastola, Nape Mnauye Mbunge na Mtama (CCM).
Ameshauri serikali kutafuta msaada kwa ajili ya kufanya upelelezi wa kina ili kukomesha vitendo hivi vya uhalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!