Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yazidi kumtekenya Magufuli, wasema anahusika kumdhuru Lissu
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yazidi kumtekenya Magufuli, wasema anahusika kumdhuru Lissu

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeituhumu serikali ya rais John Magufuli kuwa inahusika na tukio la shambulio la kifo dhidi ya Tundu Lissu, anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika mtaa wa Ufipa Kinondoni jijini Dar es salaam, Benson Kigaila, Mkurugenzi wa Mafunzo wa chama hicho amesema kuwa kuna baadhi ya matukio ambayo yanathibitisha kuwa serikali inahusika.

Amesema kauli ya Rais Magufuli aliyoitoa mwaka jana akiwa katika maadhimisho ya miaka 36 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani wa Singida kwamba ifikapo mwaka 2020 hakutakuwa na upinzani nchini.

“Lakini hakuishia hapo.baada ya pale yakaanza matamko ya kuzuia shughuli za vyama vya kisiasa jambo ambalo ni kinyume cha sheria zilizopo, lakini cha pili, wakaanza kukamatwa watu mbalimbali, yeyote anayeikosoa serikali ya Magufuli, ameishia kwenye mikono ya dola. na Lissu amekuwa mahabusu, amekuwa mahakamani kila uchwao,” aliongeza Kigaila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!