SERIKALI imeombwa kuangalia uwezekano wa kutenga maeneo kwa ajili ya ufugaji mkubwa kwa kutumia mashamba pori yaliyotaifishwa kutoka kwa wakulima walioshindwa kuyaendeleza ili kupunguza migogoro ya ardhi, anaandika Christina Haule.
Hayo yamesemwa leo na mwenyekiti wa baraza la ardhi la kijiji cha Mikese, wilayani Morogoro, Abdalah Maseni kwenye mdahalo ulioandaliwa na shirika la Uluguru Mountains Morogoro Agricultural Development Project (UMADEP ) kupitia
PELUM Tanzania , uliokuwa ukijadili nini mchango wa baraza la kijiji na mpango wa matumzi bora ya ardhi ulivyosaidia kupunguza migogoro ya ardhi vijijini.
Amesema kuwa kufuatia serikali kuwa imerejesha mikononi mwake mashamba mengi kutoka kwa wawekezaji ni bora ikatafuta baadhi ya mashamba makubwa na kutengenezea miundombinu rafiki kwa wafugaji .
Leave a comment