Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda

Halima Mdee (mwenye nguo nyeupe) akiwa mahakamani akisubiri kesi yake kutajwa kabla ya kuhairishwa
Spread the love

KESI inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), imepigwa kalenda hadi Oktoba 11,mwaka huu itakapoanza kusikilizwa, anaandika Hellen Sisya.

Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli.

Anadaiwa kutoa maneno hayo mwezi July mwaka huu, akiwa katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na anatetewa na mawakili watatu wakiongozwa na Wakili msomi Peter Kibatala huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na mawakili wawili wakiongozwa na wakili msomi, Mutalemwa Kishenyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!