Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yazidi kumtekenya Magufuli, wasema anahusika kumdhuru Lissu
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yazidi kumtekenya Magufuli, wasema anahusika kumdhuru Lissu

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeituhumu serikali ya rais John Magufuli kuwa inahusika na tukio la shambulio la kifo dhidi ya Tundu Lissu, anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika mtaa wa Ufipa Kinondoni jijini Dar es salaam, Benson Kigaila, Mkurugenzi wa Mafunzo wa chama hicho amesema kuwa kuna baadhi ya matukio ambayo yanathibitisha kuwa serikali inahusika.

Amesema kauli ya Rais Magufuli aliyoitoa mwaka jana akiwa katika maadhimisho ya miaka 36 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani wa Singida kwamba ifikapo mwaka 2020 hakutakuwa na upinzani nchini.

“Lakini hakuishia hapo.baada ya pale yakaanza matamko ya kuzuia shughuli za vyama vya kisiasa jambo ambalo ni kinyume cha sheria zilizopo, lakini cha pili, wakaanza kukamatwa watu mbalimbali, yeyote anayeikosoa serikali ya Magufuli, ameishia kwenye mikono ya dola. na Lissu amekuwa mahabusu, amekuwa mahakamani kila uchwao,” aliongeza Kigaila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!