Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime
Habari za Siasa

Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime

Spread the love

ESTER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini anashikiliwa na polisi wilayani Tarime kwa mahojiano, anaandika Hamisi Mguta.

Imeelezwa kuwa Bulaya amekamatwa kwa kosa la kuhutubia mkutano wa hadhara katika jimbo la Tarime, ambalo si jimbo lake jambo ambalo linakwenda kinyume na agizo la Rais.

Wabunge Esther Matiko na John Heche wameongozana naye kufika katika ofisi ya RCO.

Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chadema ameiambia MwanaHALISI Online kuwa Bulaya amekamatwa na yuko kituo cha polisi Tarime Rorya kuhojiwa ni kwanini aliudhuria mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Tarime vijijini uliofanyika jana nyamongo.

“Mikutano ya hadhara inafanyika kwa mujibu wa sheria na sheria haimzuii mtu yoyote kuhudhuria  mikutano ya kisiasa, kama mikutano yetu inaudhuriwa hadi na watu wa CCM, sembuse Ester Bulaya ambaye ni Mjumbe kwenye Kamati Kuu ya chama?,” alihoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!