Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Kubenea asikitishwa na mlundikano wanafunzi
Habari za Siasa

Mbunge Kubenea asikitishwa na mlundikano wanafunzi

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, akizungumza na uongozi wa shule ya msingi Kawawa, iliyopo Kata ya Mabibo
Spread the love

SAED Kubenea Mbunge wa Ubungo jijini Dar es Salaama, amesikitishwa na kuwapo msongamano wa wanafunzi katika shule ya Msingi Kawawa, anaandika Faki Sosi.

Msongamano huo unatokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo.

Kubena akiwa katika shule hiyo iliyopo kata ya Mabibo, alishuhudia msongamano wa wanafunzi shuleni hapo ambapo wanafunzi 3100 ambao wanatumia vyumba 32 wakati mahitaji ni vyumba 64.

Mbunge huyo alifika katika shule hiyo baada ya kuombwa na uongozi wa kamati ya shule kuja kuangalia sehemu litakapojengwa jengo la utawala wa shule hiyo na kusikiliza kero mbalimbali.

Mbunge huyo akizungumza na kamati ya shule, aliahidi kuchangia gharama za chakula kwa ajili ya wafanyakazi watakaofyatua matofali ili kurahisha ujenzi wa jengo hilo.

Wanafunzi wa darasa la saba wakiwa darasani

Wakati huo huo Kubenea ameushari uongozi wa shule kuangalia uwezekano wa kujenga majengo ya ghorofa ili kukabaliana na uhaba wa maeneo.

Katika ziara hiyo, Kubenea alipata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa darasa la saba wanaojiandaa na mitihani yao ya taifa na kuahidi kuwalipia ada watoto watatu wa kwanza watakaofaulu mitihani yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!