Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Kubenea asikitishwa na mlundikano wanafunzi
Habari za Siasa

Mbunge Kubenea asikitishwa na mlundikano wanafunzi

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, akizungumza na uongozi wa shule ya msingi Kawawa, iliyopo Kata ya Mabibo
Spread the love

SAED Kubenea Mbunge wa Ubungo jijini Dar es Salaama, amesikitishwa na kuwapo msongamano wa wanafunzi katika shule ya Msingi Kawawa, anaandika Faki Sosi.

Msongamano huo unatokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo.

Kubena akiwa katika shule hiyo iliyopo kata ya Mabibo, alishuhudia msongamano wa wanafunzi shuleni hapo ambapo wanafunzi 3100 ambao wanatumia vyumba 32 wakati mahitaji ni vyumba 64.

Mbunge huyo alifika katika shule hiyo baada ya kuombwa na uongozi wa kamati ya shule kuja kuangalia sehemu litakapojengwa jengo la utawala wa shule hiyo na kusikiliza kero mbalimbali.

Mbunge huyo akizungumza na kamati ya shule, aliahidi kuchangia gharama za chakula kwa ajili ya wafanyakazi watakaofyatua matofali ili kurahisha ujenzi wa jengo hilo.

Wanafunzi wa darasa la saba wakiwa darasani

Wakati huo huo Kubenea ameushari uongozi wa shule kuangalia uwezekano wa kujenga majengo ya ghorofa ili kukabaliana na uhaba wa maeneo.

Katika ziara hiyo, Kubenea alipata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa darasa la saba wanaojiandaa na mitihani yao ya taifa na kuahidi kuwalipia ada watoto watatu wa kwanza watakaofaulu mitihani yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!