Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime
Habari za Siasa

Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime

Spread the love

ESTER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini anashikiliwa na polisi wilayani Tarime kwa mahojiano, anaandika Hamisi Mguta.

Imeelezwa kuwa Bulaya amekamatwa kwa kosa la kuhutubia mkutano wa hadhara katika jimbo la Tarime, ambalo si jimbo lake jambo ambalo linakwenda kinyume na agizo la Rais.

Wabunge Esther Matiko na John Heche wameongozana naye kufika katika ofisi ya RCO.

Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chadema ameiambia MwanaHALISI Online kuwa Bulaya amekamatwa na yuko kituo cha polisi Tarime Rorya kuhojiwa ni kwanini aliudhuria mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Tarime vijijini uliofanyika jana nyamongo.

“Mikutano ya hadhara inafanyika kwa mujibu wa sheria na sheria haimzuii mtu yoyote kuhudhuria  mikutano ya kisiasa, kama mikutano yetu inaudhuriwa hadi na watu wa CCM, sembuse Ester Bulaya ambaye ni Mjumbe kwenye Kamati Kuu ya chama?,” alihoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!