Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wapiga debe Dar jino kwa jino na Polisi
Habari Mchanganyiko

Wapiga debe Dar jino kwa jino na Polisi

Lucas Mkondya, Kaimu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda maalum ya jijini Dar es Salaam limeahidi kupambana na wapiga debe katika vituo mbalimbali vya mabasi na kuwakamata, anaandika Irene Emmanuel.

Hayo yamesemwaka leo na Kamanda wa Polisi kanda hiyo, Lucas Mkondya na kewamba kazi ya kuwasaka wapiga debe imeanza katika vituo vya mabasi.

Akizungumza na MwanaHALISI online, Mkondya amesema kuna mbinu nyingi ambazo watazitumia kupambana na wapiga debe hadi kuhakikisha wameondoka wote.

Amesema hawezi kusema mbiunu watakazotumia katika kufanikisha kazi hiyo, lakini akaahidi kwamba haitakuwa na kikomo.

‘Tukiwatoa huku wakajidanganya kukimbilia mtaani watakutana na sisi tena, kwa hiyo wao wafanye kazi zilizo halali na siyo za uhalifu kwani tutapambana nao.,” Mkondya ameeleza.

Amesema tayari wameishaanza kazi katika baadhi ya vituo vya mabasi ikiwemo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Hii siyo mara ya kwanza jeshi la polisi kupiga marufuku uwepo wa wapiga debe katika vituo vya mabasi bila mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!