Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wapiga debe waiangukia serikali
Habari Mchanganyiko

Wapiga debe waiangukia serikali

Spread the love

ZAIDI ya vijana 200 ambayo wanaopiga debe eneo la Kamanga Ferry jijini Mwanza, wameiangukia serikali na kuiomba iwaache waendelee na shughulzao na kusitisha mpango wake wa kutaka kuwaondoa hapo, anaandika Moses Mseti.

Vijana hao wametoa kilio chao kwa Katibu wa Umoja na Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), mkoa wa Mwanza, Mariam Amiri.

Mwenyekiti wa wapiga debe hao, Husein Manyika, amesema baada ya kusikia tangazo la serikali kupitia vyombo vya habari ambalo linawataka kuondoka na kuacha kazi hiyo, limewashtua na kwamba hawajui pa kwenda.

Amesema kuwa katika eneo hilo pia wapo wapiga debe, wachuuzi wa samaki pamoja na wafanyabiashara wadogo maarufu kama Wamachinga.

“Tunaambiwa tuondoke hapa (Kamanga), wakati serikali haijatuandalia maeneo ya kutupeleka hivyo kabla hawajatuondoa, wanapaswa kukaa na watafakari ni wapi watakapotupeleka ndipo wachukue uamuzi huo,” amesema Manyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!