Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Wapiga debe waiangukia serikali
Habari Mchanganyiko

Wapiga debe waiangukia serikali

Spread the love

ZAIDI ya vijana 200 ambayo wanaopiga debe eneo la Kamanga Ferry jijini Mwanza, wameiangukia serikali na kuiomba iwaache waendelee na shughulzao na kusitisha mpango wake wa kutaka kuwaondoa hapo, anaandika Moses Mseti.

Vijana hao wametoa kilio chao kwa Katibu wa Umoja na Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), mkoa wa Mwanza, Mariam Amiri.

Mwenyekiti wa wapiga debe hao, Husein Manyika, amesema baada ya kusikia tangazo la serikali kupitia vyombo vya habari ambalo linawataka kuondoka na kuacha kazi hiyo, limewashtua na kwamba hawajui pa kwenda.

Amesema kuwa katika eneo hilo pia wapo wapiga debe, wachuuzi wa samaki pamoja na wafanyabiashara wadogo maarufu kama Wamachinga.

“Tunaambiwa tuondoke hapa (Kamanga), wakati serikali haijatuandalia maeneo ya kutupeleka hivyo kabla hawajatuondoa, wanapaswa kukaa na watafakari ni wapi watakapotupeleka ndipo wachukue uamuzi huo,” amesema Manyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!