Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lukuvi awacharukia viongozi wa mitaa
Habari za Siasa

Lukuvi awacharukia viongozi wa mitaa

William Lukuvi, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi (kulia waliosimama) akizungumza wananchi wa Ubungo
Spread the love

WILLIAM Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nchini, amekemea vitendo vya uonevu vinavyofanywa na viongozi wa serikali za mitaa kwa kushirikiana na matapeli kuwanyonya wananchi, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza leo katika eneo la Kimara, Kilungule wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, alipokabidhi hati 4000 za ardhi kwa wakazi wa eneo hilo, amewataka viongozi wa serikali za mitaa kuacha kutumia vyeo vyao vibaya.

“Baadhi ya viongozi wa mitaa mnatumia vibaya sana vyeo vyenu, mnauza mali za maskini, mnaotoa taarifa kwa matapeli kwamba mwenye kiwanja hiki kafa alafu mnatoa vibali wakati mnajua eneo hili ni bwana fulani na wakati ananunua mlitia sahihi.” amesema Lukuvi.

“Kesi nyingi ninazoona unakuta mtu amevamiwa shamba lake, lakini huyo mvamizi amesaidiwa na mwenyekiti wa mtaa yuleyule aliyetia sahihi kumuuzia mtu mwingine, hiyo tabia lazima ikome.” anaongeza.

Lukuvi, amewataka viongozi wa wilaya kufanya ukaguzi ili kuhakikisha kuwa sheria inafuatwa katika umiliki wa viwanja na ujenzi na siyo kujenga kiholela.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!