Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lukuvi awacharukia viongozi wa mitaa
Habari za Siasa

Lukuvi awacharukia viongozi wa mitaa

William Lukuvi, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi (kulia waliosimama) akizungumza wananchi wa Ubungo
Spread the love

WILLIAM Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nchini, amekemea vitendo vya uonevu vinavyofanywa na viongozi wa serikali za mitaa kwa kushirikiana na matapeli kuwanyonya wananchi, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza leo katika eneo la Kimara, Kilungule wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, alipokabidhi hati 4000 za ardhi kwa wakazi wa eneo hilo, amewataka viongozi wa serikali za mitaa kuacha kutumia vyeo vyao vibaya.

“Baadhi ya viongozi wa mitaa mnatumia vibaya sana vyeo vyenu, mnauza mali za maskini, mnaotoa taarifa kwa matapeli kwamba mwenye kiwanja hiki kafa alafu mnatoa vibali wakati mnajua eneo hili ni bwana fulani na wakati ananunua mlitia sahihi.” amesema Lukuvi.

“Kesi nyingi ninazoona unakuta mtu amevamiwa shamba lake, lakini huyo mvamizi amesaidiwa na mwenyekiti wa mtaa yuleyule aliyetia sahihi kumuuzia mtu mwingine, hiyo tabia lazima ikome.” anaongeza.

Lukuvi, amewataka viongozi wa wilaya kufanya ukaguzi ili kuhakikisha kuwa sheria inafuatwa katika umiliki wa viwanja na ujenzi na siyo kujenga kiholela.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!