Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bendera azifunda halmashauri zake Manyara
Habari Mchanganyiko

Bendera azifunda halmashauri zake Manyara

Joel Bendera, Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Spread the love

HALMASHAURI ya Wilaya ya Simanjiro, imeendelea kupata hati safi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini (CAG), kwa mwaka wa saba mfululizo, anaandika Mwandishi Wetu.

Akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya CAG ya mwaka wa fedha wa 2015/2016, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera, aliitaka halmashauri hiyo kutobweteka baada ya kupata hati safi badala yake waongeze juhudi zaidi.

Amesema pamoja na kuipongeza halmashauri ya wilaya kwa kupata hati safi hataki kuona kwenye mkoa wake halmashauri isiyotunza hesabu zake ipasavyo na kusababisha kupata hati chafu au yenye mashaka.

“Kwenye mkoa wangu sitaki kuona halmashauri yenye kufanya mambo ya hovyo hovyo, hivyo endapo kuna viongozi ambao wanadhani watafanya kazi kwa mazoea watafute mkoa mwingine wa kwenda na siyo Manyara,” amesema

Amesema viongozi wa halmashauri hiyo wanapaswa kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inakamilishwa kwa wakati na kutekelezwa kwa ubora na kutunza vyema taarifa za fedha ili kuendelea kupata hati safi.

“Mnapaswa kutambua siku za kufuja fedha zimepitwa na wakati na kwa wale viongozi ambao bado wanafanya kazi kwa mazoea badala ya kutumia jamii inawalazimu wajichimbie shimo na kujifukia,” amesema

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Jackson Sipitieck, amesema kwa muda wa miaka saba mfululizo wameweza kupata hati safi na wanatarajia kuendelea kupata hati safi kwa miaka ijayo ya fedha kutokana na usimamizi mzuri wa fedha waliojiwekea katika kusimamia miradi ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!