Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga
Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga

Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amewatoa hofu wananchi wa Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga kwamba hakuna mtu atakayechukuliwa ardhi yake bila kulipwa, anaandika Mwandishi Wetu

Amesema serikali haitamuonea mwananchi yeyote kwa wale ambao maeneo yao yatapitiwa na miradi mbalimbali ya uboreshaji wa miundombinu ya kiuchumi.

Waziri amesema kila mmoja atalipwa fidia kwa mujibu wa sheria ili kuipisha miradi hiyo ambayo itaisadia Tanzania kufikia kwenye uchumi wa kati mwaka (2025).

Mbarawa aliyazungumza hayo mjini Shinyanga kwenye ziara yake fupi ya ukaguzi wa miradi mbalimbali inasimamiwa na wizara anayoingoza.

Amesemma serikali imedhamiria kujenga na kufufua miundombinu yake yote ya kiuchumi, ukiwamo huo uwanja wa ndege na bandari ya Isaka wilayani Kahama, miradi ambayo itasaidia kukuza sekta ya uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!