Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa UVCCM wang’ata na kupuliza Mwanza
Habari za Siasa

UVCCM wang’ata na kupuliza Mwanza

Shaka Hamidu Shaka, Kaimu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM)
Spread the love

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umewataka viongozi wa wilaya kuwachukulia hatua watendaji wao wa chini wanaotoa mikpo kwa vikundi hewa, anaadika Mwandishi Wetu.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Shaka Hamdu Shaka.

Shaka amewataka Wakuu wa wilaya na Wakurugenzi wao kuwachukulia hatua kali watendaji walio chini yao kwa kuwa vitendo hivyo vinarudisha nyuma maendeleo.

Akizungumza katika ziara yake ya siku saba mkoani Mwanza ambayo imeanzia wilaya za Magu na Ukerewe, Shaka amesema vijana wengi wanashindwa kupata mikopo.

Amesema watendaji wa umma wamekuwa ni tatizo katika kutoa mikopo ya asilimia tano ambayo serikali imekuwa ikitenda kwa vijana na wanawake.

Amesema bado kuna urasimu mkubwa kwa maofisa wanaohusika kutoa mikopo, wanatakiwa kufanya kazi kwa vitendo ili kumuunga mkono rais Magufuli.

Sakata la Makinikia kupunguza kiwango cha Ushuru wa huduma mara mbili kuliko kilichokuwa kinatoa awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!