Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Maisha Elimu DC Muheza apiga marufuku mitihani siku za Ibada
Elimu

DC Muheza apiga marufuku mitihani siku za Ibada

Wwanafunzi wa shule ya sekondari ya Muheza High School
Spread the love

SERIKALI wilayani Muheza mkoani Tanga imepiga marufuku shule zote za msingi na sekondari wanafunzi kufanyishwa mitihani siku za ibada ikiwamo Ijumaa, Jumamosi na Jumapili, anaandika Mwandishi Wetu.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Muheza, Mwanasha Tumbo katika hotuba yake ya kufunga sherehe za makambi katika kanisa la Waadiventista Wasabato mtaa wa Michungwani wilayani hapa.

Tumbo ametoa agizo hilo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa Mchungaji wa Kanisa hilo, Laulent Fungomeli kwamba watoto wao wanashundwa kufanya ibada kwa kuwa wanakuwa shuleleni kwa ajili ya mitihani siku za Jumamosi.

Mkuu huyo wa wilaya amesisitiza kuwa shule zote za msingi na sekondari ni marufuku kufanya mtihani siku za ibada ikiwamo Ijumaa,Jumamosi na Jumapili.

Amesema kuwa lazima wanafunzi wafanye ibada kanisani ili kujenga taifa lenye msingi bora wa maadili wa kujua dini huku akiwataka wazazi kusimamia watoto wao katika elimu hasa watoto wa kike.

Amewataka waumini hao kudumisha amani pamoja na kumuombea rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli kwa kuwa kazi anayofanya ni kubwa ya kutumbua majipu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Wanafunzi wa St Joseph Dar wabuni Satellite

Spread the loveWANAFUNZI na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha...

Elimu

Serikali yatoa Sh. 573 mil. kukamilisha wa ujenzi sekondari ulioanzishwa na wanakijiji

Spread the love  SERIKALI kupitia Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga Sh....

Elimu

CBE yaja na kozi mpya 16 zikiwemo za ujasiriamali na uvumbuzi

Spread the loveChuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuanzia mwaka wa masomo...

Elimu

SUA kuhakikisha tafiti zinazofanywa zisiachwe kwenye makabati

Spread the love  MRATIBU wa utafiti na machapisho katika kurugenzi ya uzamiri,...

error: Content is protected !!