Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yamtangaza mrithi wa Muro
Michezo

Yanga yamtangaza mrithi wa Muro

Dismas Ten, Afisa Habari wa Yanga (katikati) akizungumza baada ya kutanganzwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa (kulia)
Spread the love

KLABU ya Yanga imemtangaza Dismas Ten kuwa Ofisa habari wa klabu hiyo ambaye anachuku nafasi ya Jerry Muro, anaandika Jovina Patrick.

Dismas ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Habari wa timu ya Mbeya City, anachukua nafasi ya Muro aliyekuwa anatumikia kifungo cha mwaka mmoja.

Muro alifungiwa kutojihusisha na habari kwa mwaka mmoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hivyo kufanya nafasi hiyo kuwa wazi kwa muda wote mpaka Dismas alipoteuliwa.

Charles Mkwasa, Katibu Mkuu wa Yanga amemtangaza Dismas kuwa Ofisa Habari cheo ambacho pia kilipewa jina la Mkurugenzi wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano.

Baada ya utangazwa kushika nafasi hiyo, Dismas amesema anafurahi kupewa nafasi hiyo na anaamini atafanya kazi vizuri kwa kushirikiana na wanahabari kwa kuwa amekuwa akifanya hivyo tangu alipokuwa katika ajira yake iliyopita.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

error: Content is protected !!