Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Risiti za mafuta kaa ya moto kwa vituo
Habari Mchanganyiko

Risiti za mafuta kaa ya moto kwa vituo

Christina Mndeme, Mkuu wa Dodoma, akishirikiana na Maofisa ya TRA Dodoma wakifunga moja kati ya vituo nane visivyokuwa na risiti
Spread the love

CHRISTINA Mndeme, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini amevifungia vituo nane vya mafuta visivyofuata sheria za utendaji wilayani hapo ikiwemo kutokuwa na mashine za kutolea risiti, anaandika Irene Emmanuel.

Katika ziara hiyo, Christina Mndeme amekagua utendaji wa vituo hivyo vya mafuta ikiwemo ulipaji kodi na utoaji wa risiti baada ya huduma kwa kufunga mashine za EFD zinazofungwa moja kwa moja kwenye pampu au mita ya mafuta.

Vituo nane kati ya tisa vimefungwa kwenye ziara hiyo kutokana na madai ya kutofuata sheria na utaratibu wa biashara wa utoaji risiti na kubaki kituo kimoja tu kinachofata sheria hizo.

Kazi hiyo ilifanywa kwa ushirikiano wa maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Dodoma mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!