Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Yanga yamtangaza mrithi wa Muro
Michezo

Yanga yamtangaza mrithi wa Muro

Dismas Ten, Afisa Habari wa Yanga (katikati) akizungumza baada ya kutanganzwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa (kulia)
Spread the love

KLABU ya Yanga imemtangaza Dismas Ten kuwa Ofisa habari wa klabu hiyo ambaye anachuku nafasi ya Jerry Muro, anaandika Jovina Patrick.

Dismas ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Habari wa timu ya Mbeya City, anachukua nafasi ya Muro aliyekuwa anatumikia kifungo cha mwaka mmoja.

Muro alifungiwa kutojihusisha na habari kwa mwaka mmoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hivyo kufanya nafasi hiyo kuwa wazi kwa muda wote mpaka Dismas alipoteuliwa.

Charles Mkwasa, Katibu Mkuu wa Yanga amemtangaza Dismas kuwa Ofisa Habari cheo ambacho pia kilipewa jina la Mkurugenzi wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano.

Baada ya utangazwa kushika nafasi hiyo, Dismas amesema anafurahi kupewa nafasi hiyo na anaamini atafanya kazi vizuri kwa kushirikiana na wanahabari kwa kuwa amekuwa akifanya hivyo tangu alipokuwa katika ajira yake iliyopita.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!