Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko ACACIA yakubali kuilipa serikali
Habari Mchanganyiko

ACACIA yakubali kuilipa serikali

Spread the love

ACACIA Mining Limited imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia sita (6%) baada ya sheria ya madini kubadilishwa, anaandika Victoria Chance.

Kampuni hiyo inayomiliki makampuni ya uchimbaji wa madini ya ACACIA nchini imekubali kulipa mirabaha hiyo iliyowekwa katika sheria mpya ya madini.

Sheria hiyo mpya imeitaka kampuni hiyo kulipa asilimia sita ya mirabaha ikiwa ni ongezeko la asilimia mbili (2%) moja ikiwa ya usafirishaji kwenda nje.

ACACIA inaendelea kufuatilia matokeo hayo ya sheria mpya katika mwanga wa maendeleo yake mapya ya madini.

Ikumbukwe kuwa sheria hiyo ya madini ilikuwa mswada mnamo mwaka 2010 na imeanza kutekelezwa mwaka huu.

Aidha, ACACIA ilidaiwa kukwepa kodi hapo awali baada ya kamati ya wakaguzi wa serikali kuwasilisha ripoti ya masuala ya madini kwa Rais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!