Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko ACACIA yakubali kuilipa serikali
Habari Mchanganyiko

ACACIA yakubali kuilipa serikali

Spread the love

ACACIA Mining Limited imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia sita (6%) baada ya sheria ya madini kubadilishwa, anaandika Victoria Chance.

Kampuni hiyo inayomiliki makampuni ya uchimbaji wa madini ya ACACIA nchini imekubali kulipa mirabaha hiyo iliyowekwa katika sheria mpya ya madini.

Sheria hiyo mpya imeitaka kampuni hiyo kulipa asilimia sita ya mirabaha ikiwa ni ongezeko la asilimia mbili (2%) moja ikiwa ya usafirishaji kwenda nje.

ACACIA inaendelea kufuatilia matokeo hayo ya sheria mpya katika mwanga wa maendeleo yake mapya ya madini.

Ikumbukwe kuwa sheria hiyo ya madini ilikuwa mswada mnamo mwaka 2010 na imeanza kutekelezwa mwaka huu.

Aidha, ACACIA ilidaiwa kukwepa kodi hapo awali baada ya kamati ya wakaguzi wa serikali kuwasilisha ripoti ya masuala ya madini kwa Rais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!