Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Risiti za mafuta kaa ya moto kwa vituo
Habari Mchanganyiko

Risiti za mafuta kaa ya moto kwa vituo

Christina Mndeme, Mkuu wa Dodoma, akishirikiana na Maofisa ya TRA Dodoma wakifunga moja kati ya vituo nane visivyokuwa na risiti
Spread the love

CHRISTINA Mndeme, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini amevifungia vituo nane vya mafuta visivyofuata sheria za utendaji wilayani hapo ikiwemo kutokuwa na mashine za kutolea risiti, anaandika Irene Emmanuel.

Katika ziara hiyo, Christina Mndeme amekagua utendaji wa vituo hivyo vya mafuta ikiwemo ulipaji kodi na utoaji wa risiti baada ya huduma kwa kufunga mashine za EFD zinazofungwa moja kwa moja kwenye pampu au mita ya mafuta.

Vituo nane kati ya tisa vimefungwa kwenye ziara hiyo kutokana na madai ya kutofuata sheria na utaratibu wa biashara wa utoaji risiti na kubaki kituo kimoja tu kinachofata sheria hizo.

Kazi hiyo ilifanywa kwa ushirikiano wa maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Dodoma mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!