Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu
Habari Mchanganyiko

TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA
Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekusanya Sh. 9.6 bilioni kutoka kwa kampuni za simu za mkononi kutokana na faini walizotakiwa kulipa baada ya kufanya usajili wa laini za simu bila vitambulisho na kutofuata utaratibu, anaandika Irene Emmanuel.

Kampuni zilizopigwa faini na TCRA kutokana na makosa hayo ya kusajili laini za wateja wa simu bila ya kuwa na vitambulisho na kutofuata utaratibu ni pamoja na Vodacom, Tigo, Zantel, Airtel, Smart na Halotel.

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA, amezitaja kampuni zilizotozwa faini hiyo na kiwango kwenye mabano ni Airtel (Sh1.08 bilioni), Smart (Sh1.3 bilioni), Vodacom (Sh945 milioni), Zantel (Sh105 milioni) na Halotel (Sh1.6 bilioni).

Mkurugenzi huyo amesema hiyo siyo mara ya kwanza kwa kampuni hizo kufanya makosa hayo, na kutolana na kurudia makosa wamepigwa faini nyingine kwa kufanya kosa mara mbili.

Kampuni zilizopigwa faini kutokana na kurudia kosa ni Airtel imetozwa Sh542 milioni, Smart (Sh37 milioni), Tigo (Sh625 milioni), Zantel (Sh52 milioni) na Halotel (Sh822 milioni).

Mhandisi Kilaba amesema kampuni hizo zimetozwa Sh. 500 milioni kila moja kwa kosa la kuathiri na kuhatarisha usalama wa umma na jamii ya Watanzania kwa kusajili laini bila kufuata utaratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!