RAIS wa zamani wa Brazil, Lula da Silva, amehukimiwa kifungo cha miaka tisa na nusu gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kupokea rushwa, anaandika Catherine Kayombo.
Silva anakuwa rais wa kwanza wa nchi hiyo kufugwa gerezani. Alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza 14 Septemba 2016.
Alidaiwa kuwa alijihusisha na rushwa katika kampuni ya umma ya mafuta ya Petrobras.
Kiongozi huyo wa aliyeiongoza Brazil kati ya mwaka 2003 na 2010 amepatikana pia na hatia ya kupokea mlungula wa zaidi ya dola za Marekani 100 milioni kwa ajili ya malipo ya ukarabati wa ghorofa ya mapumziko kwa kampuni ya ujenzi ya Brazil iitwayo OAS.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya kimataifa, rushwa aliyojihusisha nayo rais Silva, ndio kubwa katika historia ya nchi hiyo.
Jaji wa mahakama kuu ya Brazil, Sergio Moro, amesema kuwa amejiridhisha na ushahidi muhimu uliotolewa na mashuhuda wawili waliothibitishia mahakama yake kuwa Silva alipokea mamilioni hayo ya dola.
Silva alihukumiwa kwenda gerezani Jumatano ya tarehe 12 Julai 2017.
Kufuatia hukumu hiyo, Silva amesema hastahili adhabu hiyo kwa kuwa hajafanya kosa linalo sababisha kustahili hukumu hiyo. Mawakili wake wanajiandaa kukata rufaa.
Leave a comment