Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu amchongea Ngeleja Takukuru
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu amchongea Ngeleja Takukuru

Tundu Lissu, Rais wa TLS
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amemuwakia William Ngeleja, Mbunge wa Sengerema baada ya kurudisha fedha za Escrow zinazodaiwa kutakatishwa, anaandika Irene Emmanuel.

Lissu amedai kuwa, Ngeleja ni sehemu ya mafisadi wanaotumia madaraka vibaya hivo anatakiwa kushtakiwa pamoja na wengine wote walionufaika na pesa hizo, kurudisha fedha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) si suluhu kwani sio hao waliompatia fedha hizo apo  awali.

Ameeleza kuwa, kutokana na maelezo yake yanaonyesha yeye ni mla rushwa na muongo, sakata hilo ni la muda mrefu sasa na si kama amejua juzi.

“Kusema  alijua juzi kuwa fedha hizi ni kashfa, ni kutundanganya, anatakiwa kukamatwa na kushtakiwa,” amesema Lissu na kuongeza: “Nchi hii ukikamatwa umeiba ndiyo kesi imeishia hapo?Sheria ni kuwa ukikamatwa umeiba unafikishwa kwenye vyombo vya dola ukakutwa na hatia unafungwa na fedha kurudishwa.”

Aliongeza kuwa, wote walionufaika na fedha hizo wanapaswa kuwajibishwa na kumtaka rais achukue hatua kuanzia aliyeruhusu fedha hizo zitoke, kwani naye analeta maswali mengi.

Ngeleja aliwahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge na kuondolewa mwaka 2014 baada ya sakata hilo, na juzi ameripotiwa kurudisha fedha TRA alizopewa na James Rugemalira, fedha zinazodaiwa kutakatishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!