KAMPUNI ya Kuja na Kushoka Tools Manufactures Group kimezindua mashine ya kutengeneza mkaa unatokana na taka na kukaushia zao la tumbaku, anaandika Irene David.
Leonard Gabriel, Mkurugenzi wa kiwanda hicho amesema ili kukomesha tatizo la kuharibu mazingira na ukame wametengeneza mashine hiyo ili kuwasaidia Watanzania hasa wakulima wanaweza kutumia mkaa huo kuepuka matatizo hayo.
“Tumekuja na ubunifu wa mashine yenye uwezo mkubwa wa kuzalisha mkaa mbadala, yenye uwezo wa kuzalisha mkaa kilo 160 kwa saa na kuzalisha gunia zisizopungua 20 hadi 30 kwa siku,” amesema Gabriel.
Gabriel amesema njia mbadala ya kupata mkaa na wenye bei nafuu itakayomwezesha kila Mtanzania wa kawaida kumudu.
Amesema, mtambo huo mbali na kutengeneza mkaa kwa kutumia taka pia inaweza kutumika kwa kukaushia zao la tumbaku, hivyo ameiomba serikali kutamka kwa sheria kwa kila mkulima wa tumbaku kuanza kutumia tekinolojia hiyo katika ukaushaji.
“Mtambo huu pamoja na kuzuia kabisa matumizi ya kuni kukausha tumbaku pia utaongeza thamani ya mazao kwani mabaki yote ya mazao yatakuwa malighafi,” amesema Gabriel.
Leave a comment