Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama
Kimataifa

Qatar yadaiwa kuwa tishio la usalama

Spread the love

MATAIFA manne ya kiarabu, yanayoongoza masharti makali dhidi ya Qatar, yanasema kuwa, hatua ya Doha kukatalia mbali masharti hayo magumu dhidi yake, inaashiria nia yake ya kuendeleza sera ya kuhujumu usalama, katika eneo la mataifa ya Ghuba, anaandika Hamisi Mguta.

Kupitia taarifa ya pamoja, Saudia , Milki za kiarabu Misri na Bahrain, zimeonya kuwa, zitatoa hatua nyingine mpya na ngumu zaidi dhidi ya Qatar.

Mataifa hayo manne yalikatisha uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar mwezi uliopita, yakidai kuwa, taifa hilo linafadhili makundi ya kigaidi duniani, kama vile kundi la Muslim Brotherhood nchini Misri, na linashirikiana na hasimu mkuu wa Saudi- Iran.

Rex Tillerson, Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, anasafiri hadi Kuwait kujadili namna ya kutanzua mtafaruku huo.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson

Qatar imerudia mara kadhaa kuwa, orodha ya masharti hayo, hayana maana kabisa, mojawepo ikiwa kufunga shirika lake la habari la Al Jazeera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!