Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea apandishwa kizimbani Dodoma
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea apandishwa kizimbani Dodoma

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), amefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Dodoma na kusomewa shtaka la kumshambulia mbunge Juliana Shonza wa Chama Cha Mapinduzi, anaandika Dany Tibason.

Wabunge nane wa Chadema walikamatwa na polisi juzi mjini Dodoma kwa madai ya kumshambulia Shonza ambaye ni mbunge wa viti maalum (CCM) mkoa wa Songwe, hata hivyo baada ya mahojiano ni Kubenea pekee aliyefikishwa kortini.

Waliokamatwa na kuhojiwa ni pamoja na Pauline Gekul, Suzan Kiwanga, Joseph Selasini, Saed Kubenea, Frank Mwakajoka, Cecil Mwambe na wengine wawili.

Kubenea anadaiwa kufanya shambulizi la kudhuru mwili, kinyume cha kifungu Na. 240 cha Sheria ya Makossa ya Jinai sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Akisoma mashtaka hayo mbele ya James Karayemaha, hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Wilaya, Wakili wa serikali Beatrice Nsana ameiambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo tarehe 3Julai mwaka huu, katika viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo, Kubenea anayetetewa na mawakili watano ambao ni Jeremiah Mtobesya, James Ole Millya, Fred Kalonga, Izack Mwaipopo na Dickson Matata alikana kosa hilo.

Hakimu Karayemaha alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi kwa sharti la kuwa na mdhamini mmoja mwenye kitambulisho, barua kutoka serikali ya mtaa na Sh. 1 milioni.

Kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika kesi hiyo itatajwa tena tarehe 26 Julai mwaka huu.

Baada ya kesi hiyo kuahirishwa, Freeman Mbowe Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani amewaeleza wanahabari kuwa ni kilichofanyika ni mwendelezo wa kuwafedhehesha na kuwadhalilisha wabunge wa upinzani.

“Spika ameshabikia kitendo hiki na kusema anaruhusu wabunge wa Chadema washtakiwe kwa kosa la kubuni. Bila hata uchunguzi majina ya watu waliopo bungeni na wasiokuwepo bungeni kama Cecil Mwambe ambaye hakuwepo kabisa hata Dodoma wakadai naye alimpiga Shonza.

“Leo wamemtafuta mbunge mmoja (Kubenea) na kumshtaki kama chambo, lakini hakuna mbunge hata mmoja wa Chadema aliyemshambulia Shonza,” amesema Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!