Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mapigano ya wakulima, wafugaji yamchosha Kikwete
Habari MchanganyikoTangulizi

Mapigano ya wakulima, wafugaji yamchosha Kikwete

Mwigulu Nchemba, Waziri wa Mambo ya Ndani, akiangalia athari zilizotokana na mapigano ya wakulima na wafugaji
Spread the love

MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM) ameitaka serikali kueleza namna ilivyojipanga kupambana na janga la mapigano baina ya wakulima na wafugaji, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali bungeni leo, mbunge huyo amesema mapigano hayo yamekuwa yakisababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu.

“Je, serikali imejipangaje kupambana na janga hili?” alihoji Kikwete

Akijibu swali hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alikiri kuwepo kwa migogoro hiyo kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo kadhaa ndani ya nchi ambayo yamesababisha watanzania kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu.

Amesema katika kukabiliana na hali hiyo serikali kupitia jeshi la polisi inaendelea kushauri mamlaka zinazosimamia matumizi bora ya ardhi kutenga maeneo yatakayotumiwa na wakulima na wafugaji ili kuepusha migogoro hiyo.

Lakini pia Nchemba amesema serikali inatoa elimu kwa wakulima na wafugaji juu ya matumizi bora ya ardhi.

“Aidha jeshi la polisi hufanya doria na misako na kukamata mifugo inayoingia katika mashamba ya wakulima vitendo ambavyo vinasababisha migogoro ya mara kwa mara na kuhatarisha amani,” amesema Nchemba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!