Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mapigano ya wakulima, wafugaji yamchosha Kikwete
Habari MchanganyikoTangulizi

Mapigano ya wakulima, wafugaji yamchosha Kikwete

Mwigulu Nchemba, Waziri wa Mambo ya Ndani, akiangalia athari zilizotokana na mapigano ya wakulima na wafugaji
Spread the love

MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM) ameitaka serikali kueleza namna ilivyojipanga kupambana na janga la mapigano baina ya wakulima na wafugaji, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali bungeni leo, mbunge huyo amesema mapigano hayo yamekuwa yakisababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu.

“Je, serikali imejipangaje kupambana na janga hili?” alihoji Kikwete

Akijibu swali hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alikiri kuwepo kwa migogoro hiyo kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo kadhaa ndani ya nchi ambayo yamesababisha watanzania kupoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu.

Amesema katika kukabiliana na hali hiyo serikali kupitia jeshi la polisi inaendelea kushauri mamlaka zinazosimamia matumizi bora ya ardhi kutenga maeneo yatakayotumiwa na wakulima na wafugaji ili kuepusha migogoro hiyo.

Lakini pia Nchemba amesema serikali inatoa elimu kwa wakulima na wafugaji juu ya matumizi bora ya ardhi.

“Aidha jeshi la polisi hufanya doria na misako na kukamata mifugo inayoingia katika mashamba ya wakulima vitendo ambavyo vinasababisha migogoro ya mara kwa mara na kuhatarisha amani,” amesema Nchemba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!