Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani
Kimataifa

Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani

Spread the love

SERIKALI ya Kenya na Tanzania zimeungana kwa pamoja kulinda rasilimali za asili zilizoko katika mipaka ya nchi hizo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter jana tarehe 15 Januari 2019, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba ameandika kuwa, makubaliano hayo aliyasaini yeye pamoja na Waziri wa Mazingira na Misitu wa Kenya, Keriako Tobiko tarehe 29 Novemba 2018.

January ameandika kuwa, katika utekelezaji wa makubaliano hayo, wataangalia namna bora juu ya uhifadhi wa mazingira hasa katika maziwa ya Chala, Jipe, Natroni na Mto Mara.

Mambo mengine yatakayotekelezwa katika makubaliano hayo ni pamoja na uundwaji wa kamati ya pamoja kwa ngazi ya wizara ili kuratibu shughuli za usimamizi rasilimali za asili zilizoko mipakani, pamoja na kuanzisha timu ya wataalamu ili kutoa muongozo wa kiufundi katika usimamizi wa mipaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!