Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani
Kimataifa

Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani

Spread the love

SERIKALI ya Kenya na Tanzania zimeungana kwa pamoja kulinda rasilimali za asili zilizoko katika mipaka ya nchi hizo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter jana tarehe 15 Januari 2019, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba ameandika kuwa, makubaliano hayo aliyasaini yeye pamoja na Waziri wa Mazingira na Misitu wa Kenya, Keriako Tobiko tarehe 29 Novemba 2018.

January ameandika kuwa, katika utekelezaji wa makubaliano hayo, wataangalia namna bora juu ya uhifadhi wa mazingira hasa katika maziwa ya Chala, Jipe, Natroni na Mto Mara.

Mambo mengine yatakayotekelezwa katika makubaliano hayo ni pamoja na uundwaji wa kamati ya pamoja kwa ngazi ya wizara ili kuratibu shughuli za usimamizi rasilimali za asili zilizoko mipakani, pamoja na kuanzisha timu ya wataalamu ili kutoa muongozo wa kiufundi katika usimamizi wa mipaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!