Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watoto wenye ulemavu waomba Bima ya Afya bure
Afya

Watoto wenye ulemavu waomba Bima ya Afya bure

Spread the love

WAZAZI na walezi wenye watoto walemavu wa akili na viungo nchini wameiomba Serikali kuwakatia Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu ya watoto wao kufuatia kukabiliwa na changamoto za kiuchumi kutokana na kutumia muda mwingi kuwahudumia watoto hivyo kupunguza muda wa kufanya shughuli za kujiongezea kipato. Anaripoti Christina Haule … (endelea).

Wakizungumza wakati wa uhamasishwaji wazazi wenye watoto walemavu wa akili na viungo kutoka maeneo ya Gairo Kusini, Kilosa Kusini na Mvomero Kusini uliolenga kuelimishana namna ya malezi wazazi hao walisema kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ambaapo nyingi ya hizo zin atokana na uchumi mdogo walionao.

Mmoja wa wazazi wa watoto wenye ulemavu wa akili na viungo, Khadija Mniso mkazi wa Kilosa, amesema kuwa wanatumia muda mwingi kuwahudumia watoto hao kufuatia watoto hao mara nyingi kutokuwa na uwezo wa kusema kama wanataka kujisaidia haja kubwa ama ndogo na hivyo kuchafua nguo muda wote.

Naye Asha David Mzazi wa mtoto mwenye ulemavu amesema kuwa watoto wao wamekuwa wakinyanyapaliwa mitaani, kutengwa kwenye mikusanyiko ya watu na hivyo mara nyingi kubaki mikononi mwa wazazi au walezi wao.

Amesema kuwa kufuatia kunyanyapaliwa na kutengwa wazazi wamekuwa wakitumia muda mwingi wakiwa na wao hivyo ni vema Serikali ikawakatia Bima ya Afya ili waweze kupata matibabu.

Kwa upande wake, Ofisa Tarafa ya Mvomero, Winfred Kipako amesisitiza wazazi kuacha kuwapeleka watoto kwa waganga wa jadi pindi wanapougua kwani ulemavu mwingine unasababishwa na tiba zisizo salama.

Awali Mkurugenzi wa Shirika la Eric Memorial Foundation (EMFERD), Josephine Bakhita amesema kuwa wameamua kuwakutanisha wazazi na watoto wenye ulemavu ili kujadili changamoto zinazo wakabili na kubadilishana uzoefu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!