Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani wanne wa CUF watimuliwa Tanga
Habari za SiasaTangulizi

Madiwani wanne wa CUF watimuliwa Tanga

Spread the love

KUFUKUZWA KWA MADIWANI WETU WANNE WA TANGA!

Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, jana jioni (09 Julai 2018) ametangaza kuwafukuza udiwani, madiwani wanne wa The Civic United Front (CUF), kati yao wawili wakiwa ni madiwani wa kuchaguliwa kwenye kata (akiwemo diwani ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Wilaya ya Tanga Mjini wa chama chetu), madiwani wawili ni wa Viti Maalum.

Mkurugenzi huyo amechukua uamuzi huo baada ya kupokea barua ya Magdalena Sakaya, ambaye CCM na Dola wanamtumia ipasavyo (kupitia kwa Lipumba) ili kuhakikisha hadi mwaka 2020 maeneo ambayo CUF ina nguvu sana, madiwani na wabunge wawe wamesambaratishwa ili kuirahisishia kazi CCM.

Kwa sababu jambo hili limetokea ghafla, na likifanywa na vibaraka ambao CCM na Dola inalazimisha kuwakaimisha uongozi wa chama, mawakili wameanza hatua za kisheria ili kupambana dhidi ya jambo hilo.

Taarifa tulizonazo zinaonesha kwamba, tayari CCM na Dola vimeshaielekeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutangaza kata hizo kuwa wazi ndani ya wiki ijayo ili uchaguzi ufanyike haraka na madiwani wapya wa CCM washinde. Pia, Lipumba ametakiwa kupeleka madiwani wa viti maalum wawili haraka sana na kuhakikisha kuwa madiwani hao wanakuwa wale wanaoiunga mkono CCM.

Tanga ni jiji ambalo CUF ilishinda umeya mwaka 2015 kwa kupata madiwani wengi, kwa makusudi dola na CCM wakajitangazia kuchukua umeya ilihali aliyeshinda kwa kura za baraza la madiwani, ni diwani wa CUF (ambaye ni miongoni mwa waliotangazwa kufukuzwa jana na Mkurugenzi kwa amri ya Sakaya na Lipumba).

Mkakati wa sasa ni kama ule uliotumiwa bungeni (kesi ziko Mahakama Kuu) ambapo wabunge halali wa viti maalum wa CUF walifukuzwa uanachama na Lipumba na Sakaya na kisha kwa kasi kubwa Lipumba akateua wabunge wake binafsi wapatao nane ambao wamo bungeni hivi sasa na wote majuzi wakiiunga mkono kwa mbwembwe bajeti hewa iliyowasilishwa na serikali ya CCM (hawa ni wale wabunge ambao kila wakisimama bungeni CCM nzima inashangilia).

Nawaomba wanachama na madiwani wa CUF Tanga, ambao asilimia 99 wamekuwa na msimamo wa kukilinda chama dhidi ya wasaliti wa ndani, waendelee kuwa imara na watulivu wakati masuala haya yakishughulikiwa kwa njia za kutafuta haki ambazo zimo ndani ya uwezo wetu.

Mapambano ya ndani ya chama chetu, ya kukilinda na kukiokoa chama, yasingelichukua hata siku moja kama yasingelikuwa yanasimamiwa na na kufadhiliwa na CCM, Usalama Wa Taifa, Vyombo Dola, Serikali, Msajili wa Vyama vya Siasa n.k. tena vyombo hivyo vikifanya hivyo usiku na mchana kwa kumtumia Lipumba na genge lake.

Mapambano haya si rahisi kwa sababu tunapambaba na dola nzima na rasilimali zake zote. Nawaomba tuendelee kusimama imara mpaka haki itakapotamalaki. Haki huweza kucheleweshwa tu, haipokonyeki.

Mtatiro J,
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi,
The Civic United Front (CUF),
10 Julai 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!