KENYA imeweka rekodi katika uchaguzi mkuu mwaka huu, baada ya Tume ya Uchaguzi, kuruhusu watu waliofungwa gerezani pamoja na wale waliopo rumande kupewa nafasi ya kupiga kura, anaandika Mwandishi Wetu.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi nchini Kenya, leo asubuhi umewekwa utaratibu ambao umewawezesha wafungwa kupiga kura kama watu wengine.
Leo kuanzia asubuhi wananchi wa Kenya walijitokeza kupiga kura katika vituo mbalimbali huku wagombea nane wakichuana katika nafasi ya urais.
Wagombea urais wanaochuana kwa karibu ni Rais Odinga wa (NASA) na Uhuru Kenyatta wa (Jubilee).
Leave a comment