Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Watanzania wapewa somo hati ya kusafiria
Habari Mchanganyiko

Watanzania wapewa somo hati ya kusafiria

Spread the love

IDARA ya Uhamiaji imesema hati ya kusafiria ni haki ya kila Mtanzania ambaye anakidhi vigezo vya kuimiliki na inatolewa na serikali siyo matapeli wa mitaani, anaandikaMwandishi wetu.

Kauli hiyo imetolewa na Ofisa Uhamiaji mkoa wa Dodoma, Peter Kundy, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya maonesho ya wakulima na wafugaji nanenane kanda ya kati yaliyofanyika  kwenye viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma.

Kundy amesema kuwa licha ya kuwa hati ya kusafiria ni haki ya kila Mtanzania, lakini mwananchi huyo ni lazima awe amekidhi vigezo vinavyohitajika kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Hata hivyo, amesema wananchi wanatakiwa kuwa makini na baadhi ya watu ambao ni matapeli wanaojifanya kuwa ni maofisa Uhamiaji wakati ni uongo.

Amesema hati za kusafiria hupatikana katika ofisi za idara ya uhamiaji baada ya mtu  kujaza fomu maalumu ambazo kwa sasa zinapatikana nchi nzima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!