Kutokana na tangazo hilo, wagombea 73 wanaowania urais watalazimika kusubiri akiwemo anayetetea kiti chake Rais Muhammadu Buhari (76) anayechuana vikali na mpinzani wake mkuu, aliyekuwa makamu wa rais Atiku Abubakar (72).
Mahmood Yakubu, Mwenyekiti wa INEC alisema kuwa, kuna hitilafu za mpango uliowekwa wa ajili ya kufanya uchaguzi huo na sasa, unafanyiwa kazi ili wiki ijayo uchaguzi huo ufanyike.
“Uamuzi huu umelenga kuhakikisha uchaguzi unafanyika na kuwa huru na haki. Sasa uchaguzi utafanyika tarehe 23 Februari mwaka huu,” alisema Yakubu.
Kwenye tangazo lake hilo alisema, uchaguzi wa Ugavana, wawakilishi wa majimbo na mabaraza ya manispaa utafanyika wiki mbili baada ya uchaguzi wa rais (9 Machi 2019).
Leave a comment