Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump aichimba mkwara mzito mahakama ya ICC
Kimataifa

Trump aichimba mkwara mzito mahakama ya ICC

Donald Trump
Spread the love

UTAWALA wa Rais wa Marekani, Donald Trump umetishia kuchukua hatua kali dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), ikiwemo kuwawekea vikwazo majaji wake endapo wataendelea na uchunguzi juu ya madai ya uhalifu wa kivita uliofanywa na Wamarekani nchini Afghanistan. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Vile vile, imetishia kufunga Ofisi ya Shirika la Uhuru wa Palestina (PLO) iliyoko mjini Washington bila ya wasiwasi, kufuatia uwepo wa madai ya Palestina kujaribu kushinikiza uchunguzi wa mahakama ya ICC dhidi ya taifa la Israel ambalo ni mshirika mkubwa wa Marekani.

Mshauri wa Rais Trump kuhusu masuala ya usalama wa taifa hilo, John Bolton anatarajiwa kutoa msimamo wa Marekani mchana wa leo, ambapo kwa mujibu wa mtandao wa Reuter, umeripoti kuwa sehemu ya hotuba inayotarajiwa kutolewa na Bolton, inaeleza kwamba, Marekani iko tayari kutumia njia yoyote kulinda raia na washirika wake wanaotuhumiwa na mahakama ya ICC.

“Marekani itatumia njia yoyote itakayolazimika kutumia ili kulinda raia wetu na washirika wetu kutokana na mashtaka yasiyo ya haki na mahakama isiyo rasmi,” inaeleza sehemu ya hotuba hiyo.

Hotuba hiyo inaeleza kuwa, Marekani italipa kisasi endapo mahakama ya ICC itatekeleza azimio lake la kufungua uchunguzi huo juu ya madai ya uhalifu wa kivita uliofanywa na washirika wa Marekani pamoja na maafisa intelijensia wake katika vita iliyotokea nchini Afghanistan.

Inaelezwa kuwa, iwapo mahakama ya ICC itaendelea na msimamo wake,Marekani itazuia majaji na waendesha mashtaka wake kuingia nchini humo, pamoja na kusitisha kutoa msaada ikiwemo wa kifedha katika mahakama hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!