Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais ajiua kwa risasi kukwepa kukamatwa na Jeshi
Kimataifa

Rais ajiua kwa risasi kukwepa kukamatwa na Jeshi

Spread the love

RAIS Mstaafu wa nchi ya Peru, Alan Garcia amejiua  kwa kujipiga risasi akikwepa kuingia mikononi mwa Jeshi la Polisi la nchi hiyo, kufuatia tuhuma zilizokuwa zina mkabili za kupokea rushwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari vya kimataifa, inaeleza kwamba Garcia amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu kutokana na majeraha ya risasi, katika Hospitali ya Mji Mkuu wa Peru, Lima.

Rais wa Peru, Martin Vizcarra amethibitisha kifo cha mwanasiasa huyo aliye tawala Peru katika kipindi cha mwaka 1985 hadi 1990, na mwaka 2006 hadi 2011.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Peru, Carlos Moran amesema kabla ya Garcia kujipiga risasi, ali waambia maafisa wa polisi waliofika nyumbani kwake kwa ajili ya kumkamata, kwamba anahitaji kupiga simu kwa jamaa yake, aliporuhusiwa alikwenda kujifungia chumbani.

“Dakika chache baadae ulisikika mlio wa risasi, polisi walijaribu kufungua mlango na walipofanikiwa walimkuta Garcia akiwa katika kiti huku akiwa na jeraha la risasi kichwani,” amesema Moran.

Katibu wa marehemu Garcia, Ricardo Pinedo, amesema rais huyo wa zamani alikuwa anamiliki silaha za moto tano nyumbani kwake, na kwamba moja wapo ndiyo alitumia kumaliza uhai wake.

Jeshi la Polisi lilikuwa linamsaka  Garcia likimtuhumu kufanya kosa la kupokea rushwa enzi za utawala wake, kutoka katika kampuni ya Brazil ya Odebrecht inayoshughulika na masuala ya ujenzi.

Taarifa za vyombo vya uchunguzi nchini Peru, zinaeleza kwamba Garcia alipokea rushwa kiasi cha dola za Marekani 30 Milioni kutoka kwa kampuni ya Odebrecht.Hata hivyo, Garcia mara kadhaa alinukuliwa akikanusha tuhuma hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!