Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Museveni abadili uongozi wa jeshi
Kimataifa

Museveni abadili uongozi wa jeshi

David Muhoozi (katikati)
Spread the love

YOWERI Museveni, Rais wa Uganda amefanya mabadiliko katika jeshi la nchi hiyo kwa kumteua David Muhoozi kushika nafasi ya Mkuu wa Majeshi (CDF), anaandika Wolfram Mwalongo.

Awali, nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Edward Katumba Wamala ambapo sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Kazi nchini Uganda.

Kabla ya Muhoozi kuteuliwa katika nafasi ya CDF, alikuwa kiongozi mkuu wa jeshi la ardhi la nchi hiyo.

Katika mabadiliko hayo, Rais Museveni amemteua mtoto wake Muhoozi Kainerugaba kuwa mshauri mwandamizi wa masuala ya oparesheni maalum. Kabla ya mtoto huyo kutwaa nafasi hiyo, alikuwa mkuu wa kikosi maalumu (SDF).

SDF ni kitengo cha juu kinachomshauri rais hususani katika masuala ya kiulinzi pamoja na mambo nyeti ya taifa.

Aidha, amemteua Wilson Mbadi, aliyekuwa Mkuu wa Utumishi na Mlinzi wa rais huyo (bodyguard) kwa muda mrefu kuwa msaidizi wa CDF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!