Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Kitaifa Aliyeongoza kumng’oa  Rais al-Bashir Sudan ajiuzulu
Kitaifa

Aliyeongoza kumng’oa  Rais al-Bashir Sudan ajiuzulu

Spread the love

MKUU wa Jeshi la Sudan, Awad Ibn Auf aliyeongoza mapambano ya kumng’oa madarakani Rais wa nchi hiyo, Omar al-Bashiri amejiuzulu katika wadhifa wa uongozi wa Baraza la Jeshi linalo ongoza nchi hiyo katika serikali ya mpito ya miaka miwili. Inaripoti Mitandao ya Kijamii…(endelea).

Ibn Auf ambaye ni Waziri wa Ulinzi SudaN, ametangaza uamuzi huo leo tarehe 13 Aprili 2019 kupitia luninga ya taifa hilo, na kumtangaza msaidizi wake Luteni Generali, Abdel Fattah Abdelrahman Burhan kuwa kiongozi mpya wa Baraza la Jeshi linaloongoza taifa hilo.

Vyombo vya habari vinaeleza kuwa, waandamaji walimpinga Ibn Auf kuwa kiongozi wa baraza la uongozi la jeshi ,wakimtuhumu kwamba alikuwa ni mtu wa karibu na Rais aliyeng’olewa madarakani, al-Bashir.

Nchi ya Sudan kwa sasa iko katika miezi miatu ya dharula huku ikiongozwa na Jeshi katika serikali ya mpito ya miaka miwili.

Kwa mujibu wa jeshi hilo, katika kipindi cha usimamizi wake utafanyika mchakato wa marekebisho ya katiba ya nchi hiyo,  huku likiahidi ufanyikaji wa uchaguzi wa huru na wa haki ili kupata serikali ya wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariKitaifa

Mabasi ya New Force yapigwa kitanzi kisa ajali

Spread the loveMAMLAKA ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), imefuta ratiba za safari...

HabariKitaifa

Spika Tulia aeleza sababu za kengele ya hatari kulia Bungeni

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amesema kengele ya hatari...

HabariKitaifaTangulizi

Ni Bajeti ya kulipa madeni, mzigo wa kodi

Spread the love WAZIRI wa fedha, Mwigulu Nchemba, amewasilisha bajeti ya serikali...

Kitaifa

Serikali yatenga eka 10 kwa kila kijana mwenye sifa kufanya kilimo

Spread the love  SERIKALI nchini Tanzania imetenga eka 10 kwa kila kijana...

error: Content is protected !!