Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari Ni Bajeti ya kulipa madeni, mzigo wa kodi
HabariKitaifaTangulizi

Ni Bajeti ya kulipa madeni, mzigo wa kodi

Spread the love
WAZIRI wa fedha, Mwigulu Nchemba, amewasilisha bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2023/2024, huku sehemu kubwa ya fedha iliyotengwa ikielekezwa kwenye ulipaji wa madeni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

 Akizungumza bungeni mjini Dodoma leo Alhamisi, tarehe 15 Juni, Mwigulu alisema,katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24, serikali imepanga kutumia jumla ya Sh. 44.39 trilioni.

Kati ya fedha hizo, Sh. 6.31, zitatumika kulipia deni la taifa, huku Sh. 11.89 trilioni zikipelekwa kutoa huduma za utawala.

Katika sekta ya elimu kwa ujumla wake, serikali imepanga kutumia kiasi cha Sh. 5.95, ulinzi na usalama, Sh. 4.68 trilioni; ujenzi, usafirishaji na mawasiliano, Sh. 3.84 trilioni na nishati ikipangiwa kutumika Sh. 3.05 trilioni.

Kwa upande wa hifadhi ya jamii, serikali imetenga kiasi cha Sh. 2.35 trilioni, kilimo Sh. 1.47 trilioni, nyumba na maendeleo ya jamii, Sh. 1.34 trilioni na shughuli nyingine za maendeleo ya uchumi kumetengwa kiasi cha Sh. 1.07 trilioni.

Aidha, Mwigulu aliomba Bunge la Jamhuri, kupitisha kodi mpya ya Sh.100 kwa kila lita ya mafuta ya dizeli na petroli itakayouzwa nchini, hatua ambayo inakosolewa na baadhi ya wananchi.

“Kupata kodi ni lazima uwekeze, lakini serikali yetu haina akili hiyo ya kufanya uwekezaji mkubwa. Ndio maana kila mwaka, wanakimbilia sekta kama mafuta au pombe, maana kule ni rahisi kukusanya bila kuwekeza chochote,” anaeleza Fabian Joshua, mfanyabiashara na mkazi wa Mkuyuni, mjini Dodoma.

Anasema, “wangewekeza kwenye utalii. Kule kuna billioni za kutosha bajeti nzima ya nchi ingetoka huko. Lakini maarifa yao ndio yameishia hapo tuu na hawataki kazi ngumu.”

Naye Fatuma Juma, mkazi wa Kinodoni, Dar es Salaam, ameshutushwa na hatua ya serikali ya kuweka kodi hiyo kwenye mafuta.

Anasema,”siungi kodi hii, kwa kuwa ripoti ya Mkagugi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imeonyesha kuna wizi mkuwa wa fedha za umma, ambazo ni kodi za wananchi.”

Anaongeza, “badala ya wananchi kuongezewa kodi hii, wakati bado wana mizigo mikubwa, serikali ingejikita katika kushughulikia wizi unaofanyika.”

Hii ni bajeti ya pili, tangu Rais Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Machi mwaka juzi. Rais Samia aliapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 19 Machi 2021. Alichukua wadhifa huo kufuatia kifo cha mtangulizi wake, John Pombe Magufuli.

Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais Samia atahudumu hadi Oktoba 2025, pale uchaguzi mwingine wa urais utakapofanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!