Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ripoti ya CAG yawaweka njia panda wabunge wa CCM
Habari za SiasaTangulizi

Ripoti ya CAG yawaweka njia panda wabunge wa CCM

Spread the love

BAADHI ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi wamedai wapo njia panda, kwani hawajajua kama watachangia ripoti ya Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutokana na Spika Job Ndugai kuweka azimio kutoshirikiana na mkaguzi huyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea). 

Wabunge walio wengi ambao hawakutaka majina yao yatajwe wakati wa mahojiano maalum walisema kuwa hawajajua kama watachangia au la.

Wabunge hao kwa nyakati tofauti walisema kuwa hawajaelewa nini kitafanyika ndani ya ukumbi wa bunge wakati wa kujadili ripoti ya CAG ambayo imeishaingia bungeni na imesainiwa na CAG, Prof. Mussa Assad. 

Wabunge hao walisema kuwa wanasibiri maelekezo ya spika na kwa vyovyote vile kutakuwa na maelekezo ni namna gani ya kufanya.

Mmoja wa wabunge wa CCM alisema hali ilivyo kwa sasa pamoja na wingi wa wabunge wa CCM kupitisha azimio lakini ni dalili za uoga.

“Kilichofanyika ni kukurupuka hauwezi kutenganisha Prof. Mussa Assad na CAG sasa ripoti imeletwa bungeni na aliyesahini ni Prof.Assad hapo unaona pamekaaje,” alihoji Mbunge huyo.

Mbunge mwingine alisema kuwa mpaka sasa wabunge hawajajua nini kitafanyika na wanasubiri maelekezo ya Spika.

“Ni kweli ripoti ya CAG amewasilisha ripoti yake kwa Rais na tayari ipo bungeni iliisomwa kwa mbwembe kana kwamba hakuna kitu.

“Lakini mpaka sasa hatujajua kama tutajadili ila nadhani Spika amesafiri nadhani kamati ya maadili na sisi tutakaa katika mkutano wa chama wa wabunge wa CCM (partcoucas) na hapo tutajua cha kufanya,” alisema mbunge huyo.

Naye mbunge wa Mtera Livingiston Lusinde (CCM) alisema kuwa kwa vyovyote vile ripoti itajadiliwa.

“Ripoti itajadiliwa tu kwani kumtenga Prof. Assad na kujadili ripoti ni vitu tofauti ila itafika hatua CAG atachomoka tu,” alisema Lusinde.

Naye mbunge wa Konde Khatibu Said Haji (CUF) alisema kuwa anashukuru bunge kupokea ripoti ya CAG kwani yalikuwa malumbano makubwa kila kona.

Alisema pamoja na kuwepo kwa msemo wa funika kombe mwanaharamu apite lakini kwa ripoti ya CAG litafunikwa kombe ila mwanaharamu hatapita.

Naye mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) alisema ripoti ya CAG itajadiliwa kwani yeye amefanya kazi yake kadri alivyoweza.

Naye Mbunge wa Mbozi, Frank Mwakajoka (Chadema) alisema ni ajabu kwa wabunge wa CCM kuiogopa ripoti ya CAG.

Alisema kuwa pindi itakapofikia wakati wa kuijadili wabunge watajadili licha ya kuwa bado wabunge hawakajakabidhiwa wabunge ili waanze kuisoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!