Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zungu ataja siri Spika Tulia kushinda Urais wa IPU
Habari za SiasaTangulizi

Zungu ataja siri Spika Tulia kushinda Urais wa IPU

Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge, Azzan Zungu, amesema kilichofanya Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, achaguliwe kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ni uadilifu, kujiamini na nidhamu yake, pamoja na hatua ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kuimarisha diplomasia na mataifa ya nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Zungu ametoa kauli hiyo leo tarehe 30 Oktoba 2023, katika hafla ya kumpokea Spika Tulia, aliyewasili nchini akitokea Angola, ambapo uchaguzi ulifanyika Ijumaa iliyopita.

“Sifa za mtu kushinda hashindi sababu ya kujua, katika waliokuwa wanamsaidia Spika wanauliza kwa nini yeye tukawaambia vitu vitatu. Uadilifu, kujiamini na nidhamu. Majibu aliyokuwa anayajibu yamewafanya watu waingiwe na aibu. Wenzake walikuwa kama ni wanaharakati wakisema mtu na mikono mimi niko hivi akiulizwa swali la maana hana jibu,” amesema Zungu.

“Lakini kubwa ni Mungu na msaada kutoka kwa Rais wetu Dk. Samia, lakini yeye akajiongeza. Majibu ya mazingira anayo, haki za binadamu yapo, demokrasia duniani iko kichwani atakosa ushindi huyo?”

Dk. Tulia alishinda baada ya kupata kura 172 kati ya 303, zilizopigwa na wajumbe wa IPU, wakati washindani wake, Catherine Hara kutoka Malawi akipata kura 61.  Mergane Kanoute wa Senegal akipata kura 59, huku Abdibadhir Hagi wa Somalia, akiambulia kura 11.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!